Jumatano, 8 Juni 2016

Maisha na changamoto zake

Kukabiliana na Changamoto za Ulimwengu wa Leo



Chaguo tunazofanya—misheni, elimu, ndoa, ajira, na huduma katika Kanisa—zitajenga hatima yetu ya milele.
Mengi yameandikwa na kusemwa kuhusu kizazi cha leo cha vijana wazima. Utafiti unaonyesha kwamba wengi wanapinga dini yenye utaratibu. Wengi wana madeni na hawana ajira. Wengi wao wanapenda wazo la ndoa, lakini wengi wanaogopa kuchukua hatua hiyo. Idadi inayoongezeka haitaki watoto. Bila injili na mwongozo wenye maongozi, Wengi wanazunguka-zunguka katika njia ngeni na wanapoteza njia zao.
Kwa bahati nzuri, vijana wazima waumini wa Kanisa wamebakia nyuma katika mielekeo hii inayosumbua, kwa kiasi, kwa sababu tumebarikiwa na mpango wa injili. Mpango ule unajumuisha kushikilia kwa nguvu fimbo ya chuma—kujishikilia kwenye neno la Mungu na neno la manabii Wake. Tutashikilia fimbo ambayo inatuelekeza kurudi kwake? Sasa ni “siku ya kuchagua”1 kwetu sote.
Nilipokuwa mvulana, wakati nilipokuwa karibu kufanya uchaguzi ambao nilikuwa sijaukagua vyema, baba yangu wakati mwingine angesema, “Robert, kuwa makini na ufanye kile unachojua ni sahihi! Ninyi mmeshapitia hayo. Katika roho ya mazungumzo yake ya wazi, ningependa kusema hususani kwenu vijana—vijana waungwana—vijana wazima wetu waungwana, kwani “roho yangu hufurahia katika uwazi ... ili kwamba [tuweze] kujifunza.”2
Mnaishi katika kipindi cha muda muhimu cha maisha yenu. Chaguzi mnazofanya—misheni, elimu, ndoa, ajira na huduma katika Kanisa—zitawaletea uzoefu milele. Hii inamaanisha siku zote lazima muwe mnalenga mbele—mkilenga siku zijazo.
Kama rubani katika Jeshi la Anga, nilijifundisha kanuni hii: kamwe usiruke kwa makusudi katika mvua ya radi. (Mimi sitakwambia jinsi nilivyogudua hayo.) Badala yake izunguke, chukua njia ingine, au ngoja dhoruba iishe kabla ya kutua.
Wapendwa vijana wazima, ndugu na akina dada, Nataka kuwasaidia “kuruka kwa usahihi” wakati wa dhoruba za siku za mwisho zinapotanda. Ninyi ni marubani. Wajibu wenu ni kufikiri kuhusu matokeo ya kila uchaguzi. Jiulizeni wenyewe, "Kama nikifanya uchaguzi huu, ni kitu ngani kibaya sana ambacho kinaweza kutokea?” Uchaguzi wenu sahihi utawasaidia msichepuke kutoka kwenye mwelekeo sahihi.
Fikirieni kuhusu hilo: Kama mtachagua kutokunywa pombe, hamtakuwa mlevi! Kama kamwe hamtachagua kuwa na madeni, mtaepuka uwezekano wa kufilisika!
Mojawapo ya madhumumi ya maandiko ni kutuonyesha jinsi watu wenye haki wanajibu majaribu na uovu. Kwa kifupi, Yaepuke! Yusufu alimkimbia mke wa Potifa.3 Lehi alichukuwa familia yake na waliondoka Yerusalemu.4 Mariamu na Yusufu walikimbilia Misri kutoroka njama ovu ya Herode.5 Katika kila mfano, Baba wa Mbinguni aliwatahadharisha waumini hawa. Vilevile, Yeye atatusaidia sisi kujua kama tupigane, tukimbie, au kukubali hali zetu zinazobadilika. Yeye atanena kwetu kupitia sala, wakati tunaposali, tutakuwa na Roho Mtakatifu, ambaye atatuongoza. Tuna maandiko, mafundisho ya manabii wanaoishi, baraka za Baba mkuu, ushauri wa kutia moyo wa wazazi na viongozi wa ukuhani na makundi saidizi, na zaidi ya hao, sauti ndogo tulivu ya Roho.
Bwana daima ataweka ahadi Yake: “Nitakuongoza siku zote.”6 Swali pekee ni, tutajiachia wenyewe tuongozwe? Tutasikia sauti Yake na sauti za watumishi Wake?
Ninashuhudia kwamba kama upo hapo kwa ajili ya Bwana, Yeye atakuwepo kwa ajili yako.7 Kama unampenda Yeye na kutii amri Zake, utakuwa na Roho Wake apate kuwa pamoja nawe na kukuongoza. “Weka imani yako katika Roho yule ambaye anakuongoza kufanya mema. ... Kwa hii tutajua vitu vyote ... kuhusu vitu vya haki.”8
Pamoja na kanuni hizo kama msingi, naweza kuwapeni ushauri kiasi wa kiutendaji?
Wengi wa kizazi chenu wanakabiliwa na madeni makubwa mno. Wakati nilipokuwa kijana, Rais wa kigingi changu alikuwa Mkurugenzi wa banki ya kitega uchumi kwenye Wall Street. Alinifundisha, “Wewe ni tajiri kama unaweza kuishi kwa furaha kwa njia ambayo unatumia kidogo kuliko kipato chako. Unaweza kufanya vipi? Lipa zaka yako na kisha weka akiba! Wakati unachuma zaidi, weka akiba zaidi. Usishindane na wengine kuwa na vitu vya gharama. Usinunue kile usichoweza kukimudu.
Vijana wengi katika ulimwengu wanaingia kwenye madeni kupata elimu na baadaye wanakuta gharama ya shule ni kubwa mno kuliko wanavyoweza kulipa. Tafuta msaada wa masomo, mikopo isiyo na riba. Pata ajira ya muda, na kama inawezekana, ikusaidie kulipa gharama yako mwenyewe. Hii itahitaji dhabihu kiasi, lakini itawasaidia kufanikiwa.
Elimu hukutayarisha kwa nafasi nzuri za ajira. Huwaweka kwenye nafasi nzuri ya kuhudumu na kuwabariki wale walio karibu nanyi. Itawaweka kwenye njia kujifunza ya maisha yote. Itawaimarisha kupigana dhidi ya upumbavu na makosa. Kama vile Joseph Smith alivyofunza: “Elimu huondosha giza, wasi wasi na shaka; kwa haya hayawezi kuwepo pale elimu ilipo. ... Katika elimu kuna uwezo.”9 “Lakini kuelimika ni vyema ikiwa watatii mawaidha ya Mungu.”10 Elimu itawatayarisha ninyi kwa kile kilicho mbele, ikijumuisha ndoa.
Tena, naomba niseme wazi kabisa? Njia ile inayoelekea kwenye ndoa hupitia upeo unaoitwa miadi! Miadi ni nafasi ya mazungumzo marefu. Wakati mnafanya miadi, jifunze kila kitu kuhusu nyote wenyewe. Jifahamisheni na familia inapowezekana. Je! Malengo yenu yanambatana? Je! Mnashiriki hisia sawa kuhusu maandiko, Mwokozi, ukuhani, hekalu, ulezi, wito wa Kanisani, na kuwahudumia wengine? Je! Mshaangliana kwa makini mnapokabiliwa shida, mjibizo wa fanaka, ushinde, kujizuia ghadhabu, na kukabilia na vikwazo? Je! Yule anayefanya miadi naye uvuruga watu ama huwajenga? Je! Mtazamo na lugha na mwenendo wake ndiyo vile ungependa kuishi navyo kila siku?
Baada ya hayo yote, hakuna kati yetu anayeowa mtu aliye kamili; tunaoa mwenye uwezo. Ndoa sahihi si tu ile inayohusu nini tunataka; ni kuhusu nini anachotaka na kile—yule ambaye atakuwa mwenzi wangu—anataka na anahitaji mimi niwe.
Tukisema kwa uwazi, tafadhali usiwe na miadi katika umri wako wote wa miaka ya 20 ili tu “ujifurahishe” hivyo ukachelewesha ndoa kwa ajili ya maslahi mengine. Kwa nini?” Kwa sababu miadi na ndoa si kikomo cha safari zetu. Ni lango la kule hatimaye tunataka kwenda. “Kwa hiyo mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, na atashikamana kwa mke wake.”11
Jukumu lako sasa ni kuwa mstahiki kwa mtu unayetaka kumwoa. Kama unataka kuoa mwenye uchangamfu, anayevutia, mwaminifu, mwenye furaha, mchapa kazi, mtu wa kiroho, basi uwe mtu wa aina hiyo. Kama wewe ni mtu huyo na hujaoa bado, kuwa na subira. Msubirie Bwana. Nashuhudia kwamba Bwana anajua hamu zako na anakupenda kwa kujitolea kwako kwa imani Kwake. Ana mpango kwa ajili yako, iwe ni katika maisha haya ama yajayo. Silikiliza Roho Wake. “Usitafute kumshauri Bwana, lakini kupokea ushauri kutoka kwake.”12 Katika maisha haya au yajayo, ahadi zake zitatimizwa. “Kama umejitayarisha hutaogopa.”13
Kama hauna mali nyingi, usijali. Muumini wa ajabu wa Kanisa majuzi aliniambia, “Mimi sikuwalea watoto wangu kwa pesa; niliwalea kwa imani. Kuna ukweli mkuu katika hayo. Anza kufanya imani katika kila sehemu ya maisha yako. Kama hautafanya hivyo, utaugua kile ninachokiita “imani nyauka.” Nguvu hasa zinazohitajika kufanya imani yako zitafifia. Kwa hivyo fanya imani kila siku, na wewe atapata “nguvu kwa nguvu ... wakawa imara zaidi na imara katika imani ya Kristo.”14
Kuwa tayari kwa ndoa, hakikisheni kwamba mnastahili kupokea sakramenti na mnastahili kuwa na sifu ya hekalu. Nendeni hekaluni kila mara. Mhudumu katika Kanisa. Pamoja na miito ya Kanisa, fuateni mfano wa Mwokozi, ambaye kwa urahisi, “aliendelea kufanya mema.”15
Sasa, mnaweza kuwa na maswali ya dhati kuhusu chaguzi za huko mbele. Katika miaka ya ujana wangu, nilitafuta ushauri kutoka kwa wazazi wangu na kutoka kwa washauri waaminifu wanaoaminika. Mmoja alikuwa mwenye ukuhani; mwingine alikuwa mwalimu ambaye aliniamini. Wote waliniambia, “Kama unataka ushauri wangu, uwe tayari kuukubali. Mimi nilielewa hiyo ilimaanisha nini. Kwa maombi chagua wanasihi ambao wana usimamizi wa kweli kuhusu ufanisi wako wa kiroho. Uwe mwangalifu kuhusu kuchukuwa ushauri kutoka kwa rika lako. Kama unataka zaidi ya uliyonayo sasa, angalia juu, siyo kando kando!16
Kumbuka, hakuna anayeweza kufikia juu kwa niaba yenu. Bali imani yenu tu na maombi yatasababisha nyinyi kuwa na mabadiliko makubwa ya moyo. Uamuzi wenu tu kuwa watiifu unaweza kubadili maisha yenu. Kwa sababu ya dhabihu ya upatanisho ya Mwokozi kwa ajili yako, uwezo upo ndani yako.17 Una wakala wako, una ushuhuda thabiti kama wewe ni mtiifu, na unaweza kumfuata Roho ambaye hukuongoza.
Hivi majuzi, kijana mtengeneza filamu alisema alihisi alikuwa sehemu ya “kizazi cha wapotevu”—kizazi “kinachotafuta matumaini na shangwe na ukamilifu, lakini kutafuta katika sehemu zote mbaya na kwa njia mbaya.”18
Katika fumbo la Mwokozi la mwana mpotevu, mwana alikuwa na baraka nyingi zikimsubiri, lakini kabla hajazidai, ilibidi angalie kwa makini maisha yake, chaguo zake, na hali zake. Muujiza ambao ulitokea baadaye umeelezewa katika maandiko kwa kishazi rahisi: “Alipozingatia moyoni mwake.”19 Acha niwatie moyo mzingatie moyoni mwenu? Katika Kanisa, wakati maamuzi ya muhimu lazima yafanywe, kila mara tunakuwa na mikutano ya baraza. Mikutano ya baraza ya familia inatumikia azma sawa. Mnaweza kutaka kuendesha kile nitaita “baraza binafsi.” Tumia muda kiasi peke yako. Fikiria kuhusu mambo yaliyo mbele. Jiulize: “Ni sehemu gani za maisha yangu ninazohitaji kuimarishwa ili kwamba niweze kuwaimarisha wengine? Wapi nataka niwe wapi mwaka mmoja kutoka sasa? Miaka miwili kutoka sasa? Ni chaguzi gani ninazohitaji kufanya kufika hapo?” Kumbuka tu, wewe ndiye rubani, na ndiyo unayeshikilia usukani. Ninashuhudia kwamba unapojitambua, Baba yako wa Mbinguni atakuja kwako. Kwa mikono ya kufariji ya Roho Yake Mtakatifu, Yeye atakuongoza.
Ninatoa ushuhuda wangu kwamba Mungu yu hai. Ninatoa ushuhuda wangu maalumu kwamba Mwokozi anawependa. “Je, si lazima sisi tuendelee katika kazi hii [Yake iliyo kuu]? Twende mbele na siyo nyuma.”20 Mnapomfuata Yeye, Atawaimarisha na kuwathibitisha. Yeye atawaleta hata kwenye nyumba yenu ya juu kabisa. Katika jina la Yesu Kristo, amina

Umuimu wa fasihi ndani ya jamii

2.3 UMUHIMU YA FASIHI SIMULIZI KATIKA KIPENGELE CHA SEMI (METHALI) KATIKA JAMII HII YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.
Kwa kutumia methali za Kiswahili zilizoandikwa kwa lugha ya Picha,Tashihisi, Onomatopea/tanakali sauti na methali  za kabila la kisukuma zenye maudhui sawa katika kila methali ya lugha ya kiswahili  kuonyesha nafasi ya utanzu huu katika jamii hii ya sayansi na teknolojia kama ifuatavyo;
 
 Methali ya kisukuma;Gutu gudakilaga ntwe.
 
 Maana;Sikio halizidi kichwa.
 
 Methali yaKiswahili; Mkuza pezi ni papa nyama wote wangawako/nyama wote wangawako mkuza pezi ni papa
 
Ufafanuzi; Methali hizi ni moja na inategemeana na wewe unavyoweza kuanza kuanza au kuandika.unaweza kuanza na mkuza pezi ni papa nyama wote wangawako,au nyama wote wangawako mkuza pezi ni papa.
 Pezi ni kiungo kilichoko ubavuni na mgogoni mwa samaki,akiwemo papa .kiungo hiki kinamwezesha samaki( papa ) kwenda .
            Katika wanyama wote papa ndiye mwenyewe uwezo wa kukuza pezi .methali hii ni sawa na kusema mkuza pezi ni papa wanyama wote wangalikuwepo (wangawako)wanyama wote mkuza pezi ni papa peke yake (hata kama wanyama wote wangelikuwemo na mwenye uwezo wa kukuza pezi ni papa tu.)
 
Maana; a) Mtu pekee mwenye uwezo wa kufanya jambo miongoni mwa wengine .
            b) Mwenye uamuzi wa mwisho. (Mauya B.A,2008).
 
Umuhimu; Methali hii hutumika pale inapoelezea kuweko na mtu tu miongoni mwa walio na uwezo kwa kufanya jambo ambalo wengine hawawezi kulifanya.mfano hata wangelikuwepo wakuu wote wa nchi mwenye uwezo wa mwisho ni Rais
 
Methali ya kisukuma; Nsuji go mva gugamwiwagwa gulali nsebu.
 


 Maana; Mchuzi wa mbwa hunywewa ungali wa moto
 
Methali ya Kiswahili; Udongo uwahi uli maji.
 
Ufafanuzi; Udongo unaweza kufinyangika vizuri bila ya shida uwapo maji .Ukikauka unakuwa mgumu kufinyangika .kama mtu anataka matokeo mazuri,udongo huo ufinyangwe ungali maji ,yaani uwapo mbichi
 
Maana;Wahi kutatua tatizo kabla halijawa kubwa .kwa mfano,
Tibu maradhi kabla ya kukomaa,au wahi kuzuia jambo kabla ya kuharibika .mkanye mototo akiwa mdogo. (Mauya B.A,2008).
 
Umuhimu;Methali hii hutumika kuwapa nasaha watu wasisubiri matatizo hadi yakue .Aidha, methali hii inawaasa watu wasichelewe kushughulikia tatizo mapema ,kabla mambo hayajaharibika .ujumbe wa methali hii nikuwatanabahisha watu kuchukua tahadhari kabla ya hatari .kwa mfano kutibu maradhi kabla ya kukomaa au kuonya watoto wenye mienendo mibaya wakiwa wadogo kabla hawajaharibika  kama vile kuacha ujeuri, udukozi na ugomvi.
 
Methali ya kisukuma;Omasala adabunagwa nigo.
 
Maana;Mwelevu hashindwi kitu.
 
Methali ya Kiswahili;Kozi mwanamandanda kulala na njaa kupenda.
 
Ufafanuzi;Kozi ni aina ya ndege mdogo ambaye hutaga mayai mengi sana.kiasi kwamba mengine anaweza kuyafanya chakula na kuyala na mengine akayatotoa katika hali hii akilala na njaa anapenda, siyo kwamba hana chakula
 
Maana;Mtu mwenye nafasi na uwezo ,kupata taabu ni matakwa yake .tajiri yoyote halali na njaa , akilala na njaa amependa mwenyewe. (Mauya B.A,2008).
 
Umuhimu; Methali hii hutumika kuwaelezea watu wanaojitosheleza katika kila hali .kwao kupata taabu ni kwa kipenda wanyewe .kwa mfano kama mwanafunzi yuko kwenye shule yenye vifaa vya kutosha ,kutokusoma kwake ni kupenda kwake mwenyewe .kama unataka mchumba katika mazingira yenye wanawake na wanaume wengi ,basi kutokuoa na kuolewa ni kupennda kwako mwenyewe
 
Methali ya kisukuma; Nomolomo agagulaga kaya.
 
Maana; Muongo hachagui kabila
 
Methali ya Kiswahili; Mvungu mkeka.
 
Ufafanuzi; mvungu nisehemu yenye uwazi iliyo chini ya kitu kama vile kitanda ,meza na kiti.mkeka ni kitu kama vile jamvi linaloshonwa kutokana na kili na hutumika kwa kulalia kutandikia chini au kitandani . hapa mvungu umefananishwa na mkeka  kwa maana kuwa ,mkeka ukitandikwa chini unaweze ukaficha kitu na kisionekane , kama vile mvungu ufanyavyo..Ndio maana husema mvungu mkeka,kwani vyote vinaweza kuficha kitu na kisionekane.
 
Maana;Usidharau au jihadhari na sehemu za uficho ,kama vile mvungu kwani panaweza pakawa na kitu kilichojificha kama vili nyoka ,mtu au chochote kile ambacho kinaweza kukuletea madhara ama kile mtu anayesikiliza au kuona kile unachokitenda ukadhani ni siri. (Mauya B.A,2008).
 
Umuhimu;Methali hii hutumika kutoa onyo au kuwashauri watu wenye tabia ya kuropokaropoka ,kufanya au kuleta jambo bila kulichunguza yanayomzunguka au sehemu zenye  uficho kama vile chumbani ambamo mna kitanda .
            Hivyo basi, unapokuwa katika sehemu kama hizo lazima uangalie na uchunguze kwanza kabla hujaropoka au kukaa au kufanya jambo lolote.
 
Methali ya kisukuma;Mashi ga mbili gagakwililaga mkaya
 
Maana;Mavi ya mbuzi hujaa zizini.
 
Methaki ya Kiswahili;Ndondondo si chururu.
 
Ufafanuzi;Ndondondo ni kitu kinacho toka kidogo kidogo,kama vile maji ,mafuta .Wakati chururu ni kitu kinacho toka kwa wingi au mfululizo kwa mara moja .kwa lugha nyepesi ,ni sawa na kusema kuwa kidogokidogo kwa muda mrefu si sawa na wingi kwa mara moja.
 
Maana; a) kupata kitu kidogokidogo Kwa muda mrefu ni bora kuliko kupata kingi kwa mara moja.
            b) Kutumia akiba yako kidogokidogo na kwa muda mrefu ni bora kuliko kutumia akiba yote kwa mara moja, ikiisha utabakia na matatizo au shida. (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu; methali hii hutumika kuwaasa watu wenye tabia ya kufuja mali au kutumia pesa /chakula kwa fujo au kwa wingi, kwamba watumie mali zao kidogokidogo na kwa uangalifu.
 
Methali ya kisukuma;Gwigwa go mbulu mpaga mininga mmato.
 
Maana;Kusikia kwa kenge mpaka damu masikioni
 
Methali ya kiswahili;Kama hujui kufa chungulia kaburi.
 
Ufafanuzi;Kaburi ni shimo la kuzikia mtu aliyekufa .Wakati wa kuzika chungulia kaburi utaona kweli kuna kufa maana unaona mtu anavyozikwa.
 
Maana;kujifunza kutokana na matukio au matendo.Kwa mfano ,kama hujui UKIMWI ,kaangalie wanaougua na ukitaka kufeli angalia mtu anayecheza darasani,asiyetaka kusoma kwa bidii matokeo yake ni kufeli. (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu;Methali hii hutumika pale mtu anaposema au kutoa ushauri kwa mtu ambaye ni mbishi ;anayefanya ajizi na jambo la hatari au linaloweza kumuathiri .Aangalie kwa wale waliofanya ajizi  yaliyowatokea.
 
 Methali ya kisukuma;Uyasesilwe mbeho aditanelwagwa moto.
 
 Maana;Aliyepigwa baridi haitiwi moto.
 
Methali ya kiswahili;Mlilala handingwandingwa mwemacho haambiwi tule.
 
Ufafanuzi;Mlilala linamaanisha mtu aliyelala.kundingwandingwa ni kuwa na njaa au kusikia njaa .handingwandingwa lina maana hana njaa .mwemacho lina maana ya mwenye macho .Methali hii ni sawa na kusema? Aliyelala hana njaa na aliye macho haambiwi tule kwani chakula anakiona.
 
Maana;Asiye hangaika hana tatizo ,na mwenye tatizo haambiwi atatue ,tatzo lake (ataangaika ili alitatue.). (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu;Methali hii huwasema watu wasiotaka kujishughulisha au kujituma ili kujiletea maendeleo. Mtu ambaye hataki kujituma ili ajiletee maendeleo basi achana naye kwani hii ni kwa faida yake na mtu anayetaka maendeleo haambiwi la kufanya ili ajiletee maendeleo .Yeye mwenyewe atahangaika kujiletea maendeleo.
 
Methali ya kisukuma;Kugongola gulu gumala mimbo
.
Maana;Ukimwimbia kiziwi nyimbo unajisumbua.
 
Methali ya kiswahili;Uso wa samaki hausikii viungo.
 
Ufafanuzi;Samaki ni kiumbe kinachoishi ndani ya maji (baharini,ziwani au mtoni).Samaki hata aungweje,uso wake haubadiliki.
 
Maana;a)Mtu asiyebadilika (kitabia).
            b)Mtu asiyeshaurika.
            c)Mtu asiye sikia la mtu yoyote. (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu;Methli hii hutumika kuelezea mtu ambaye ni mgumu kubadilika,hasa katika tabia au mwenendo
 
Methali ya kisukuma;Kushema chonza mpanga ubudale
 
Maana;Kukamua kicheche mpaka ulale kifudifudi.
 
Methali ya kiswahili;Utaka cha uvunguni sharti ainame
 
Ufafanuzi;Uvunguni ni sehemu ya chini ya kitu kama vile meza,kitanda au kiti.Nidhahiri ikiwakitu kimewekwa uvunguni ili kukipata lazima uiname ,yaani usiwe mvivu kuinama.
 
Maana;Ukitaka mafanikio lazima ujitume kufanya kazi. .(Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu ;Methali hii huwashauri watu wajitume kufanya kazi
 
 Methali ya kisukuma;Nigo go ng’hala gugashililaga gwi bega.
 
Maana;Mali ya mjinga huisha bila kujua
 
Methali ya kiswahili;Mali bila daftari, hughibu bila habari.
 
Ufafanuzi;Mali ni kitu kinachomilikiwa na mtu na kinaweza kuwa kitu au fedha.Daftari ni kitu kinachowekewe hesabu za kitu au fedha na siku zote mtu makini mali yake, huweka hesabu ya mali yake kwenye daftari. Hii inamsaidia kufuata mienendo ya mali yake ili kuepuka upotevu.
 
Maana;a)mali bila kuwekea kumbukumbu kimaandishi hupotea bila ya habari.
            b)Mara nyingi ,anapata hasara asiyeweka kumbukumbu ya mali yake. (Mauya.B.A,2008)
 
Umuhimu ;Methali hii hutufundisha tuwe tunaweka mali zetu katika kumbukumbu au maandishi
 
 Methali ya kisukuma;Gulya mwa mpanga.
 
Maana;kula ni uhai.
 
Methali ya kiswahili;Ukitaka kula nguruwe chagua aliyenona.
 
Ufafanuzi;Kwa waislamu kula nguruwe ni haramu Kwa mujibu wa dini yake mwislamu kakatazwa kula nguruwe,Inapotokea,kwa makusudi,mwislamu kula nguruwe ,na kuvunja imani hiyo,inaaonekana ni vizuri basi, mtu wa namna hiyo ale nguruwe aliyenona.Haimkini mtu kuvunja imani kwa kula nguruwe aliyekonda kwa kwenda kinyume cha dini.
 
Maana; a) Unapotaka kufanya jambo linaloweza kukuletea madhara,ulifanye kikwelikweli au kwa dhati.
b) Ukitaka kufanya ambo fanya kwa dhati.
            c) Ukiamua kufanya jambo liwe la heri au la shari fanya kwa bidii na nguvu zote (fanya kikwelikweli katika kiwango cha juu). (MauyaB.A,2008).
 
Umuhimu; Methali hii hutumika pale mtu anapoamua kufanya jambo kwa makusudi ,jambo ambalo litamletea madhara ,basi anapaswa kulifanya kwa mafanikio ya hali ya juu.
 
Methali ya kisikuma; Gugulu guli ng’ombe, idako ilalija.
 
Maana; Mtembezi hula miguu yake na mkaaji hulala njaa.
 
Methali ya Kiswahili; Mgaaga na upwa hali wali mkavu.
 
Ufafanuzi; kugaagaa ni kugeukageuka katika hali ya kujilaza. Hapa kugaagaa imetumika kumaanisha kutembeatembea
Upwa ni kandokando ya bahari ambapo maji hujaa na kupwa. Mara nyingi, sehemu kama hizi hupatikana samaki ambao wamesukumwa na maji na kuachwa mchangani
Mgaagaa na upwa ni sawa na kusema hali wali mkavu ni sawa na kusema anaetembeatembea kando kando ya bahari hali wali mkavu, maana anaweza akaokota hata kisamaki au kidagaa na kupata kitowewo.
 
Maana; Anayefanya juhudi katika kazi, masomo au jambo lolota hufanikiwa. (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu; Methali hii hutumika katika kuwahimiza au kuwashauri watu wafanye bidii katika shughuli zao na watafaniliwa. Wasijikalie tu.
 
 Methali ya kisukuma; Gukungila nungu gwelwang’holo
 
Maana; kuwinda nungunungu ni jambo la maana
 
Methali ya Kiswahili;kata  pua uunge wajihi.
 
Ufafanuzi; kata pua uunge wajii ni sawa na kutoa kijinofu cha pua na kukuunga kwenye sehemu nyingine ya uso iliyoharibika iliionekane nzuri. Kwa maana nyingine ni kutoa au kupunguza kitu mahali na kwenda kufidia pengine.
 
Maana; Linda hadhi au heshima yako hatakama itakugalimu . Unaweza kupunguza kiasi fulani cha mali au pesa ili uilinde hiyo heshima kwa mfano kama mtu anakaribiwa na tatizo ambalo kama hatalitatua litamfedhehesha. Mtu mwenye njaa, kesi au deni, ita mbidi, hafanye chini juu au aende mbio, hatakama kuuza au kuweka poni baadhi ya mali zake atatue tatizo hilo ili asihathilike. Anapouza na kuweka poni baadhi ya mali zake ndipo anapokata pua na kuunga wajii yaani kuilisnda heshima. Hii inamaana mtu hawezi kubaki na shida kama anacho kitu ambacho anaweza kukibadili kwa njia yoyote ili atatue hiyo shida. Huwezi ukawa unadeni la kukuathili wakati uacheleani au baiskeli ndani ya nyumba na usiwezw kuuza au kuweka rehani na kutatua tatizo hilo, maana kifaacho mtu ni chake, kata pua uunge wajihi. (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu ; methali hii huwashauri watu watumie malizao au asilimali zao katika kutatua matatizo yao, wasipate taabu wakati wanavyo vitu vya kuwasaidia katika matatizo yao.
 
Methali ya kisukuma; Lubigi lo kule  ludabulagaga.
 
Maana;Fimbo ya mbali haiui
 
Methali ya kiswahili;Hamadi kibindoni silaha iliyo mkononi
 
Ufafanuzi;Hamadi ni neno linalotokana na mahamad(Mtume).pia ni neno linaloonyesha mshtuko au kitendo cha ghafla .Kibindoni ni ndani ya mkunjo wa nguo .kama vile shuka au kikoi ,unaokunjwa mithili ya mfuko na mara nyingi hutumika kuwekea fedha.Hivyo basi kibindoni ni kama mfuko wa kuwekea fedha,kwa maana hiyo basi ,methali hii ni sawa na kusema kwa  jina la muhamad  kuwa na pesa kibindoni ni sawa na kuwa na silaha mkononi pale inapohitajika.hadhari ni mfukoni au kitu ulichonacho .
 
Maana;kuwa na pesa mfukoni ni sawa na kuwa na silaha mkononi pale inapoitajika (mbele ya adui).Pia ni sawa na kusema pale mtu anapopatwa na tatizo lolote kile kitu kitakachokusaidia ni kile kilicho mbele yako;awe mtu ,kitu au kifaa chochote kile .mathalani umepatikana na tatizo na linahitajika kutatuliwa kwa pesa.pesa itakayokusaidia ni ile uliyo nayo hapa hapo ulipo iwe ndani ya mfuko au mkononi,kuliko ile ambayo ipo mahali pengine ,kama vile iliyo benki, nyumbani au kwa mtu mwingine ingawa ni yako.hali kadhalika kama umetokewa na adui yako ghafla silaha itakayo kusaidia ni ile iliyopo mkononi na siyo ile iliyo mahali pengine .
Kwa maana nyingine kitakacho kusaidia ni kile kilichoko mbele yako yaani kile ulichonacho hapohapo kuliko kilicho mbali na wewe .hata ukivamiwa na adui wa kukusaidia ni jirani yako au yoyote yule atakayekuwa karibu yako kwa wakati ule. (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu; methali hii hutoa hadhari kwa mtu ajiwekee akiba au awe na uhusiano mzuri na majirani zake na hajihadhari na lolote na kwa wakati wowote ,yaani asijisahau kila waksti awe amejitayarisha kwa lolote lile.
 
Methali ya kisukuma; kulanga shelangile ukwikumya na bulangi
 
Maana; kufundusha kinachofundishika utajivuna unajua kufundisha
 
Methali ya Kiswahili; kutwanga nisile unga nazuia mchi wangu
 
Ufafanuzi;ni kuponda kitu,kama vile mtama au mahindi katika kinu kwa kutumia mchi ili kutoa punje.Baada ya kutwanga punje huweza kufundwa na kutoa unga wa kula .inapotokea mtwangaji hapati ule unga basi anaweza kukata tamaa kutwanga na hivyo kuzuia mchi wake ,kwa maana hatwangi tena. 
 
Maana; Mtu asipotuzwa au kufaidika kwa kazi anayoifanya anaweza asiendelee kufanya kazi hiyo au mtu asipopata motisha au malipo atapunguza juhudi za kazi au kuacha kabisa kufanya kazi hiyo. (Mauya B.A,2008)
 
Umuhimu; Hutumika kutoa onyo kwa watu ambao hawapendi kutoa malipo/ujira unaostahili kwa aliyefanya kazi au kutoa shukran kwa mtu aliyemtendea mema
 
 
 
 

 

  

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama
  
  
This Blog
Linked From Here
Wavuti nizisomazo
The Web
This Blog
 
 
 
Linked From Here
 
 
 
Wavuti nizisomazo
 
 
 

 Tulitembelea makazi ya kwanza walipofikia Wakristu wa kwanza kutua kwenye kisiwa cha Ukerewe zaidi ya miaka 100 iliyopita. Hakuna maelezo mengi sana kuhusu eneo hili ila simulizi za mauaji yaliyofanyika hapo dhidi ya baadhi ya wageni hao na mtawala wa eneo hilo wa wakati huo. Ni eneo ambalo liko kwenye kilima chenye mwinuko mkubwa unaowezesha kuona umbali mkubwa juu ya Ziwa Viktoria. Mwenyeji wangu aliniambia kuwa nyakati ambapo hakuna ukungu yawezekana kuona ndege zikipaa na kutua kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.
Ukerewe ni kisiwa chenye mandhari za kuvutia na visiwa vingi vinavyokizunguka. Upande wa kulia wa picha kinaonekana kisiwa cha Bwiru.
Baada ya hapo tulitembelea eneo la ufukweni wa ziwa ambapo mjasiria mali mmoja wa Nansio, makao makuu ya wilaya ya Ukerewe, anajenga hoteli itakayozingatia utunzwaji wa mazingira wa eneo hilo.

Taarifa ijayo: Watanzania ni watu wakarimu

sehemu ya kwanza ya makala hii
sehemu ya tatu ya makala hii

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

This Blog
Linked From Here
Wavuti nizisomazo
The Web
This Blog
 
 
 
Linked From Here
 
 
 
Wavuti nizisomazo
 
 
 
The Web
 
 
 

Saturday, September 6, 2014

Mila na tamaduni: Watanzania ni wakarimu (sehemu ya pili)

Hivi karibuni nimemaliza mzunguko wa kazi na mazoezi nikitumia baiskeli wa takriban kilomita 174 ndani ya mikoa ya Mwanza na Mara. Imenipa fursa ya kuthibitisha kuwa utamaduni wa ukarimu miongoni mwa Watanzania bado uko imara.

Jiunge nami kwenye sehemu ya pili ya msafara huu...

Agosti 2
Tulitembelea makazi ya kwanza walipofikia Wakristu wa kwanza kutua kwenye kisiwa cha Ukerewe zaidi ya miaka 100 iliyopita. Hakuna maelezo mengi sana kuhusu eneo hili ila simulizi za mauaji yaliyofanyika hapo dhidi ya baadhi ya wageni hao na mtawala wa eneo hilo wa wakati huo. Ni eneo ambalo liko kwenye kilima chenye mwinuko mkubwa unaowezesha kuona umbali mkubwa juu ya Ziwa Viktoria. Mwenyeji wangu aliniambia kuwa nyakati ambapo hakuna ukungu yawezekana kuona ndege zikipaa na kutua kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.
Ukerewe ni kisiwa chenye mandhari za kuvutia na visiwa vingi vinavyokizunguka. Upande wa kulia wa picha kinaonekana kisiwa cha Bwiru.
Baada ya hapo tulitembelea eneo la ufukweni wa ziwa ambapo mjasiria mali mmoja wa Nansio, makao makuu ya wilaya ya Ukerewe, anajenga hoteli itakayozingatia utunzwaji wa mazingira wa eneo hilo.

Taarifa ijayo: Watanzania ni watu wakarimu

sehemu ya kwanza ya makala hii
sehemu ya tatu ya makala hii

No comments: